IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ WAHARIRI kisiwani Pemba wametakiwa kuwasimamia vyema waandishi wao kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi, ili habari zao zilete mafanikio katika jamii. Akizungumza na wahariri katika Ukumbi wa TAMWA Chake Chake Pemba, Afisa Mawasiliano kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Zanzibar (TAMWA), Sophia Ngalapi alisema kuwa, waandishi wengi tayari wameshapewa mafunzo kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa kupitia mradi wa kupambana na Mabadiliko ya tabianchi (ZanAdapt), hivyo ni jukumu la wahariri kusimamia ili ziandikwe habari zenye ubora. Alisema kuwa, kupitia sauti za wanahabari, wanaamini kwamba zitaisaidia jamii hasa wanawake katika kukabiliana na mabadiliko ya hali ya tabianchi ambayo huathiri sana maendeleo katika maeneo wanayoishi. "Mabadiliko ya hali ya hewa yanaleta athari mbali mbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, hivyo kupitia kalamu za waandishi wataibua changamoto na kupatiwa ufumbuzi unaofaa kwa maslahi yao na taifa kwa u...
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI WANAWAKE WAMEJITOKEZA, VYAMA VIWATEUE.TAREHE: 27/07/2025. Wadau wa masuala ya wanawake na uongozi wanaviomba vyama vya siasa kuhakikisha kuwa vinawateua wanawake waliokidhi vigezo, kugombea nafasi za uongozi ndani ya vyama vyao kwenye uchaguzi wa ushindani ndani ya nafasi za uwakilishi, ubunge na udiwani....